Jinsi ya kujiunga na UTT AMIS

UTT AMIS

Jinsi ya kujiunga na UTT AMIS: UTT AMIS ni taasisi ya Serikali ya Tanzania iliyo chini ya Wizara ya Fedha ambayo dhumuni lake kuu ni kuanzisha na kuendesha mifuko ya uwekezaji wa pamoja hapa nchini ili kuwawezesha wananchi wengi zaidi kujiwekea akiba na kuwekeza katika masoko ya fedha na mitaji.

Bei ya vipande vya UTT AMIS 2024: Changamoto kubwa iliyopo ni kwamba bado hali ya utamaduni wa kuweka akiba na kuwekeza katika masoko ya fedha na mitaji bado iko chini kwa sababu za kihistoria, kijamii, kiuchumi na wakati mwingine sababu huwa ni kipato kidogo na mahitaji ni mengi. Ukweli unabaki ya kuwa hakuna siku fedha zinaweza kutosha.

Hivyo inamlazimu kujenga nidhamu na tabia ya kujiwekea akiba ya fedha kutokana na kipato anachapata. Siyo jambo rahisi kuweza kuweka akiba ya fedha, lakini ili uweze kufanya hivyo ni muhimu kujenga nidhamu katika matumizi yetu.

Jinsi ya kujiunga na UTT AMIS

Afisa Masoko na Uhusiano wa UTT AMIS, Rahim Mwanga anasema “Suala si kuweka akiba na kuwekeza tuu, ila tunatakiwa kuweka akiba na kuwekeza kwa ufanisi ambao ni Uwekezaji unaozingatia kuwa na malengo, kuweka mpango wa kufikia malengo na muda. Mfano lengo ni kuwa na milioni 5, kwa muda wa miaka 3 na utawekeza kila mwezi. Hiyo ndiyo itakayo kuwa dira ya kukuwezesha kufika malengo.

Jinsi ya kujiunga na UTT AMIS

Fomu ya Maombi

Afisa Masoko na Uhusiano wa UTT AMIS, Rahim Mwanga anasema, “Siku zote ukiwa na akiba ya fedha unatakiwa kuziwekeza. Uwekezaji ni dhana pana, kwa mfano, mwingine anataka kununua kiwanja, mwingine aanzishe biashara, mwingine ampeleke mtoto shule, mwingine akasome yeye mwenyewe, lengo likiwa ni kwamba ile fedha ya akiba ilete matokeo chanya kwake. Hata hivyo, inatakiwa ieleweke kwamba kuna muda kati ya kuweka akiba, kuwekeza na kutimiza lengo.

See also: