Alikiba azindua kituo cha redio inaitwa ‘Crown FM’

Alikiba azindua kituo cha redio inaitwa ‘Crown FM’ – Staa wa Bongo Fleva, Alikiba amezindua kituo cha redio kiitwacho “Crown FM”. Uzinduzi huo ulifanyika usiku wa Jumamosi Machi 9, 2024 katika hoteli ya Hyatt Regency jijini Dare es Salaam katika kusherehekea miaka 20 ya Kiba kwenye muziki.

Akizungumza katika hafla hiyo, Kiba alieleza kuwa vyombo vya habari ni muhimu kwa sababu vimemkuza mwanamuziki na anakumbuka kuwa alipewa zawadi ya redio ndogo na baba yake alipokuwa mdogo.

Pia mwimbaji huyo alisema changamoto alizozipata zimemtia moyo pia kuanzisha kampuni ya vyombo vya habari ambayo ina kituo cha redio na televisheni.

Crown FM, ambayo itarusha matangazo yake kwa masafa ya 92.1 FM, inapatikana katika jiji la Dar es Salaam, kisiwani Zanzibar, Tanga pamoja na eneo la pwani nchini Tanzania.

Sherehe za miaka 20 ya kuzaliwa kwa Ali Kiba, zilihudhuriwa na viongozi wengi maarufu nchini Tanzania akiwemo Rais mstaafu Jakaya Kikwete, Nape Nauye Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Albert Chalamila, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mwigulu Chemba ambaye ni Waziri wa Fedha na Ridhiwani Kikwete. Mbunge wa Chalinze.

Alikiba azindua kituo cha redio inaitwa ‘Crown FM’

Alikiba azindua kituo cha redio inaitwa 'Crown FM'
Alikiba azindua kituo cha redio inaitwa ‘Crown FM’

See also:

  1. Ratiba ya Klabu Bingwa Robo fainali 2023/2024 CAF
  2. Jinsi ya kuangalia deni la gari online 2024
  3. TETESI ZA USAJILI: Dube anukia Jangwani
  4. Dube Afichua Mahovu ya Uongozi wa Azam FC