Goli la Yanga dhidi ya Mamelodi Lenye utata

Goli la Yanga dhidi ya Mamelodi Lenye utata

Goli la Yanga dhidi ya Mamelodi Lenye utata, Gumzo linaloendelea hapa South Africa kwenye mitandao ni kwamba Yanga ndio wameshinda mechi lakini Mamelodi ndio walionufaika.

Goli la Yanga dhidi ya Mamelodi Lenye utata

Nikiweka ushabiki wangu pembeni Mimi huwa napenda Sana kujifunza Vitu nisivyovijuwa.

South Africa wapinzani ni Chiefs na Orlando, lakini ukiwafuatilia vizuri unakuta wote wameungana kumshutumu Motsepe na kuilaani Mamelodi.

Inshort Ile Support ambayo kocha wa Mamelodi amelalamika haipati sasa ndio hatoipata kabisa hasa Kwa Wazulu wa Johannesburg, mechi za nusu fainali good option wakacheze Cape town watapata full support Kwa sababu Cape town hizi mechi za Champions league timu za Cape town hazina ubavu wa kutobowa.

Mashabiki wengi wa South Africa wanauliza, kama refa alikwenda kuangalia VAR ili ampe Kadi nyekundu Lomalisa, ni Kwa nini hakwenda kuangalia VAR kuhusu goli?

Ushauri wangu Yanga watume malalamiko rasmi CAF, refa aadhibiwe hizo pesa za Motsepe ndio ajikimu nazo, ila matokeo ya uwanjani huwa hayabadirishwi na Mimi si muumini wa ushindi wa mezani.

See also: