Jinsi ya kujiunga na bima ya afya NHIF

Jinsi ya kujiunga na bima ya afya NHIF | Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) ni Taasisi ya Bima ya Afya ya Jamii iliyoanzishwa chini ya Sheria ya Taifa ya Bima ya Afya, Sura ya 395 kwa lengo kuu la kuhakikisha upatikanaji wa huduma za afya kwa watu. Ni taasisi ya Serikali inayofanya kazi chini ya Wizara ya Afya (MOH).

Usimamizi wa Mfuko ni wa Bodi ya Wakurugenzi huku shughuli zake za kila siku zikisimamiwa na Mkurugenzi Mkuu. Hazina inachukulia bima ya afya kama jambo la kijamii badala ya hitaji la mtu binafsi na hivyo kufanya kazi chini ya kanuni za kushiriki hatari na mshikamano miongoni mwa wanachama.

Pamoja na utaratibu wa uandikishaji wa lazima kwa watumishi wa umma, Mfuko umeongeza wigo wake na kujumuisha vikundi vingine kama Madiwani, kampuni binafsi, taasisi za elimu, watu binafsi, watoto chini ya umri wa miaka 18, wakulima katika vyama vya ushirika pamoja na vikundi vilivyosajiliwa kama Machinga na Vikundi vya bodaboda. Mfuko pia unasimamia Mpango wa Bima ya Afya ya Bunge na unashughulikia Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar.

Majukumu ya msingi ya Mfuko ni:-

  • Kusajili wanachama na kutoa vitambulisho;
  • Kukusanya michango;
  • Kuthibitisha watoa huduma za afya kwa ajili ya kutoa huduma za afya kwa wanachama;
  • Urejeshaji wa madai ya watoa huduma za afya;
  • Wekeza fedha za ziada zilizokusanywa ili kupata mapato;
  • Kufanya Tathmini na Uthamini wa Hali halisi; na
  • Kutoa elimu ya bima ya afya kwa umma.

Jinsi ya kujiunga na bima ya afya NHIF

Utaratibu wa ujazaji wa Fomu za Bima ya Afya (NHIF)

Idadi ya watu wanaotakiwa kujazwa kwenye fomu ya bima ya afya ni 16 kwa mtiririko ufuatao;

Mchangiaji mwenyewe na mwenza wake(mke au mme)

Faili ya watoto wasiozidi 4 chini ya miaka 18,au wazazi/wakwe katika idadi hiyo ya watu wane(40 maana unaweza ukawajaza watoto wawili(2) na wazazi (2).

1. VIAMBATANISHO

Mchangiaji:

1.Hati ya kupokelea mshahara(salary slip) yenye makato ya bima ya afya.

2.Picha zenye ukubwa wa pasipoti(passport size) moja ya hivi karibuni.

Mwenza(Mke au mme)

1.Nakala ya  cheti cha ndoa (copy)

2.Picha zenye ukubwa wa pasipoti(passport size) moja ya hivi karibuni.

Watoto:

1.Nakala ya Vyeti vya kuzaliwa(copy).

2. Picha zenye ukubwa wa pasipoti(passport size) moja ya hivi karibuni.

Wazazi:

1.Cheti cha kuzaliwa cha mchangiaji (mtumishi).

2 Picha zenye ukubwa wa pasipoti(passport size) moja  ya hivi karibuni

Jinsi ya kujiunga na bima ya afya NHIF

Wakwe:

  1. Cheti cha ndoa
  2.  Picha zenye ukubwa wa pasipoti(passport size) moja ya hivi karibuni

•Kuongeza mtegemezi:

Viambatanisho ni vilevile saraly slip,picha pasporti size na nakala ya cheti cha kuzaliwa.

Utalipia benki Tzsh 20,000/=kwa kila kadi iliyopotea kwa akaunti namba 61010016954 yenye jina Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya.

Baada ya hapo utamwona Mratibu ukiwa na loss Report ya polisi,pay slip ya benki uliyolipia na picha passport size ili ujaze fomu nyingine uweze kupata kadi nyingine.

Kwa wastaafu:

Viambatanisho

1.Nakala ya kibali cha kustaafu

2.Unarudisha kodi ulizopewa pamoja na wategemezi wako.

3.Picha yako passport size pamoja na ya mwenza wako ya hivi karibuni ili uandaliwe kadi nyingine.

4.Kama kuna kadi zimepotea kati ya kadi sita(6) ulizopewa,utaripoti kwa mratibu wa Bima ya Afya au Afisa Utumishi ili uandikiwe barua ya kwenda nayo polisi.

See also:

Jinsi ya kujiunga na JKT 2024/2025

Jinsi ya kupata namba ya NIDA kwa haraka