Mchungaji Dkt. Msigwa kahamia CCM na Kutambulishwa leo, KIKAO CHA HALMASHAURI KUU YA CCM TAIFA Kimtambulisha Mchungaji Dkt. Msigwa Kama Mwanachama Mpya
Kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kilichofanyika leo chini ya uongozi wa mwenyekiti wake ambaye pia ni Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kimemtambulisha rasmi Mchungaji Dkt. Msigwa kuwa mwanachama mpya wa chama hicho. Mkutano huo muhimu umefanyika kwa mafanikio, ukihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa chama na wadau wa kisiasa.
Dkt. Msigwa, ambaye ni mchungaji na mwanazuoni, amejiunga na CCM akileta uzoefu na mtazamo mpya ndani ya chama. Ujio wake unatarajiwa kuimarisha zaidi chama kwa kutoa mchango wake katika nyanja mbalimbali za maendeleo na uongozi. Uamuzi wa kumkaribisha Dkt. Msigwa unadhihirisha nia ya CCM ya kuendelea kujijenga na kuleta mabadiliko chanya kwa manufaa ya taifa zima.
![Mchungaji Dkt. Msigwa kahamia CCM na Kutambulishwa leo](https://kijiweforum.com/wp-content/uploads/2024/06/msigwa-1024x658.png)
Mchungaji Dkt. Msigwa kahamia CCM na Kutambulishwa leo
Hii video inatueleza mengi kupitia body language
Mmegundua kitu?— Maria Sarungi Tsehai (@MariaSTsehai) June 30, 2024
ALIYEKUWA Mwenyekiti wa Chadema kanda ya Nyasa, Mchungaji Peter Msigwa amejiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kutambulishwa katika kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM (NEC).
Mchungaji Msigwa aliyewahi kuwa mjumbe wa kamati kuu ya Chadema, akitambulishwa leo Jumapili Juni 30, 2024 katika kikao kilichofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam, kikiongozwa na Mwenyekiti wa CCM, Rais Samia Suluhu Hassan.
Katibu Mkuu wa CCM, Dk Emmanuel Nchimbi ndiye aliyemshika mkono Mchungaji Msigwa na kuingia ndani ya ukumbi waliokuwepo wajumbe wa NEC.
SEE ALSO:
- Wafungaji Bora Copa America 2024, Top goal scorers
- Lautaro anaendeleza mfululizo wa kufunga Copa América
- Canada Yafuzu Robo Fainali ya CONMEBOL Copa América
- 8 Players Kaizer Chiefs Have Been Linked to Signings
- Kaizer Chiefs confirm six departures for 2024/25 Season
- USAJILI SIMBA, Fadlu Davids kujiunga na Simba kama kocha mkuu
- Mamelodi Sundowns offer Feisal as New Signing 2024-25
- Orlando Pirates Set to Sign TS Galaxy’s Ncwadi Saki
- USAJILI AZAM, Nassor Saadun ajiunga na Azam kutokea Geita Gold
- Ratiba ya Ligi Kuu Tanzania 2024/2025 NBC Premier League
Leave a Reply