Steven Mukwala kujiunga na Simba SC baada ya kuondoka Asante Kotoko

Steven Mukwala kujiunga na Simba SC baada ya kuondoka Asante Kotoko | MSHAMBULIAJI Raia wa Uganda, Steven Mukwala yuko mbioni kusajiliwa na vigogo wa Tanzania, Simba SC baada ya mkataba wake na Asante Kotoko kumalizika.

Taarifa kutoka katika nchi hiyo ya Afrika Mashariki zinasema kuwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 yuko tayari kusaini mkataba wa miaka mitatu na klabu hiyo na kupata mshahara mnono kufuatia sifa yake ya kuwa mfungaji mahiri katika Ligi Kuu ya Ghana.

Mazungumzo na Simba yameripotiwa kuwa katika hatua za juu, ambapo Mukwala anatazamiwa kupokea kitita cha dola 130,000 na mshahara wa kila mwezi wa dola 9,000.

Steven Mukwala kujiunga na Simba SC baada ya kuondoka Asante Kotoko, Mukwala alijiunga na Porcupine Warriors mwaka wa 2022 na amekuwa na mchango mkubwa, akifunga zaidi ya mabao 25 ​​katika mechi 65 za ligi.

Mshambulizi huyo mwenye umri wa miaka 24 alifunga mabao 14 katika mechi 28 za Ligi Kuu ya Ghana msimu wa 2023-2024, na kuisaidia Kotoko kumaliza katika nafasi ya sita katika ligi ya timu 18.

Steven Mukwala kujiunga na Simba SC baada ya kuondoka Asante Kotoko
Steven Mukwala kujiunga na Simba SC baada ya kuondoka Asante Kotoko

Aling’ara kwenye Super Clash dhidi ya mahasimu wao Accra Hearts of Oak SC, akifunga katika mechi zote mbili, likiwemo la marudiano la mkondo wa pili kwenye Uwanja wa Baba Yara. Katika msimu wake wa kwanza, Mukwala alifunga mabao 11 na kutoa asisti tano katika mechi 31 za ligi.

Steven Mukwala kujiunga na Simba SC baada ya kuondoka Asante Kotoko

SEE ALSO: