Fountain Gate Wanaendeleza Ubabe NBC Ligi Kuu

Fountain Gate Wanaendeleza Ubabe NBC Ligi Kuu

Fountain Gate Wanaendeleza Ubabe NBC Ligi Kuu | Waifunga na Kuitesa Kagera Sugar kwa Ushindi wa 3-1.

Fountain Gate FC wameendelea kuonyesha ubora wao katika Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara kwa kuwachapa Kagera Sugar mabao 3-1 katika mchezo uliochezwa leo. Ushindi huu ni ishara kuwa timu hii imejiimarisha vyema na inapaswa kuzingatiwa kama moja ya vikosi vinavyoweza kutoa ushindani mkubwa msimu huu.

Goli la mapema lilifungwa na nyota wao Selemani Mwalimu katika dakika ya 6, likifuatiwa na bao la pili la Salum Kihimbwa katika dakika ya 12, na kuweka Fountain Gate mbele kwa magoli mawili dhidi ya wapinzani wao. Kipindi cha pili kiliendelea kuwa cha moto ambapo Obrey Chirwa aliifungia Fountain Gate bao la tatu katika dakika ya 49, huku Elie Mokono akiwapatia Kagera Sugar goli la kufutia machozi katika dakika za nyongeza 90+3′.

Fountain Gate Wanaendeleza Ubabe NBC Ligi Kuu
Fountain Gate Wanaendeleza Ubabe NBC Ligi Kuu

Mashabiki wa Fountain Gate wana kila sababu ya kufurahia uchezaji wa timu yao, hasa kwa winga wao mahiri Selemani Mwalimu, ambaye ameonyesha kuwa ni “mwalimu” kweli, akiiongoza timu yake kwa ustadi mkubwa na kupachika bao muhimu.

Ushindi huu unaendelea kuiweka Fountain Gate katika nafasi nzuri kwenye msimamo wa ligi, huku wakijipambanua kama timu inayoweza kushindana na vigogo wa ligi kama Yanga, Simba, na Azam FC. Ikiwa wataendelea na kiwango hiki, bila shaka watajiweka kwenye kinyang’anyiro cha kutafuta nafasi ya juu msimu huu.

Timu ya Kagera Sugar, licha ya kushindwa, ilionyesha juhudi ya kurudi kwenye mchezo, lakini safu yao ya ulinzi ilizidiwa nguvu na Fountain Gate waliokuwa na ari ya ushindi.

ANGALIA PIA: